



Wazazi na walezi kote nchini wametakiwa makini kuhakikisha watoto wao hawatembei ovyo usiku wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili kuwaepusha kubakwa.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake nchini (Tamwa), Ananilea Nkya, ilisema kuwa, takwimu zinaonyesha idadi ya watoto wanaobakwa huongezeka mara dufu nyakati za mfungo wa Ramadhani.