


Hospitali ya TMJ ya jijini Dar es Salaam imetangaza kupanua huduma zake kwa kufunga vifaa vya teknolojia ya kisasa ikiwemo mashine ya kufanya vipimo vya kichwa aina ya MRI.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Tayabali Jafferji, vifaa vingine ni CT-Scanner na X-Ray, kufunga vifaa vya kisasa kwenye chumba cha upasuaji na maabara.
Kufungwa kwa mashine hiyo kunafanya idadi yake kufikia ya pili kwa hospitali binafsi nchini, kwa kuwa ilikuwa ikipatikana Muhimbili pekee.