Saturday May 25, 2013
| Text Size
[-]
[+]
Search IPPmedia

Kampuni ya Uingereza kuthamini mali za Uda

9th May 2012
Print
Comments

Kampuni ya kimataifa ya Uhasibu na Ukaguzi wa Mahesabu ya KPMG, ya Uingereza imeteuliwa kufanya tathmini ya mali za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) ikiwa ni makubaliano ya kumaliza  mgogoro muda mrefu wa ubinafusishaji wa shirika hilo.

Serikali  serilikubaliana na mwekezaji  kampuni ya Simon Group  kuthamini maliza za shirika hilo ili kwenda sawa na soko.

Meneja Mawasiliano wa Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya umma (CHC), Joseph Mapunda, amethibitisha kuwepo kwa makubaliano hayo kati ya serikali na Simon Group, na kwamba CHC imeiteua kampuni ya  KPMG yenye tawi lake nchini.

“Kwa sasa siwezi kukueleza chochote kuhusu utamini kwani bado haujakamilika na sisi CHC na tukikabidhiwa ripoti ya uthamini toka KPMG tutawaeleza,” alisema Mapunda.

Mkurugenzi wa KPMG Keton Shar alipoulizwa kuhusu zoezi hili alisema hawezi kusema lolote kwani kazi haijamalizika.

“Lakini wewe unajua kuwa sisi hatuwezi kuzungumza kazi za wateja wetu bila wao kuturuhusu ili ni kweli kazi tunaifanya ikimalizika tutapeleka ripoti kwa mteja wetu nae atawapa majibu,” alisema mkurugenzi huyo.


SOURCE: NIPASHE
0 Comments | Be the first to comment