Saturday May 25, 2013
| Text Size
[-]
[+]
Search IPPmedia

Viongozi wanne wa CWT watiwa mbaroni

1st August 2012
Print
Comments

Viongozi wanne wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) katika baadhi ya wilaya mkoani Mbeya wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuhamasisha walimu wenzao kushiriki katika mgomo wa walimu ulioanza juzi nchini, huku watu tisa wakishikiliwa na Jeshi hilo kwa tuhuma za kushiriki vurugu ubwa zilizotokea jana katika mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, alisema jana kuwa viongozi wa CWT waliokamatwa walikuwa wakishirikiana na watu wengine kupita kwenye shule mbalimbali mkoani Mbeya kuwashinikiza walimu wanaoendelea kufundisha ili washiriki kwenye mgomo wa walimu.

Aliwataja viongozi hao kuwa ni Katibu CWT Wilaya ya Kyela, Patro Mangula (52); Katibu wa CWT Wilaya ya Rungwe, Akson Kibona na wajumbe wawili wa wa CWT Wilaya ya Ileje ambao ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Mbebe, Emmanuel Kyejo (45) na Mwalimu wa Shule ya Msingi Mkumbukwa, Anyakingwe Lwingwa (54).

Alisema watuhumiwa wote baada ya kamatwa walifikishwa mahakani kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kuhusu vurugu zilizosababisha kuvunjwa kwa ofisi ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya mji mdogo wa Tunduma, Kamanda Diwani alisema kuwa baada ya upelelezi kufanywa na Jeshi la Polisi, watu tisa wametiwa mbaroni kuhusiana na vurugu hizo

Watuhumiwa hao ni Meck Mbilinyi (52), Akida Kondo (25), Charles Lupia (29), Athuman Mgala (39), Stella Gilbert (20), Atilio Mnyamwanga (28), Nicodemus Mnyamwanga (17), Mashaka Kyusa (27) na James Kabuje (29), wote wakazi wa mji mdogo wa Tunduma.

Alisema pia Jeshi la Polisi limefanikiwa kuokoa baadhi ya mali zilizoibwa katika ofisi za Mamlaka ya Mji huo ambazo alizitaja kuwa ni mabati 168, printa moja, mita mbili za maji, bendera moja ya Taifa na mashine moja ya kurufu.

Wakati huo huo, mgomo uliendelea jana na baadhi ya walimu kutofika kabisa shuleni huku wale wanaofika wakisaini kitabu cha mahudhurio na urejea majumbani.

Wanafunzi katika shule mbalimbali walikuwa wakicheza nje ya shule huku wengine wakirandaranda mitaani.

SOURCE: NIPASHE
0 Comments | Be the first to comment