


.jpg)
Kamati Kuu (CC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imeteua majina 32 ya makatibu wa wilaya.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, aliwataja walioteuliwa ambao hawajapangiwa wilaya kuwa ni Grayson Mwangu, Abdallah Hassan, Ernest Makunga, Mgen Haji na Innocent Namzabar.
Wengine ni Nicholaus Malema, Mercy Moleli Michael Bundala, Elisante Kimaro, Zacharia Mwansasu, Eliud Semauye, Habas Mwijiki, Loth Ole Nesele, Charles Sangura, Donald Magessa na Fredrick Sabuni.
Nape aliwataja wenyeviti wengine kuwa ni pamoja na Janrth Mashele,Daniel Porokwa, Zongo Lobe Zongo, Mwanamvua Kilo, Joyce Mmasi, Simon Yaawo, Epimack Makuya, Amina Kinyogoto, Asia Mohammed, Venosa Mjema, Augustine Minja , Elly Minja, Ernest Machunda, Selemani Majilanga, Chritina Gukwi na Joel Kafunge Mwakila.
Aidha, Jana Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete wakati akifungua semina ya katiba aliwataja wajumbe wa Nec kuwa makini ili kupata Katiba Mpya itakayosaidia pia kujenga imani kwa chama hicho.