Sunday May 26, 2013
| Text Size
[-]
[+]
Search IPPmedia

Serikali: Hakuna fedha za kuwalipa Tazara

14th May 2012
Print
Comments
Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu.

Sakata la wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (Tazara) limechukuwa sura nyingine baada ya Serikali kugoma kuwalipa mishahara kwa maelezo kuwa shirika linatakiwa kujiendesha lenyewe.

Awali Chama cha wafanyakazi wa Reli (Trawu) kilitoa tamko na kuipa Serikali siku tano kuwalipa wafanyakazi mishahara kutokana na uongozi wa Tazara kushindwa kutekeleza ahadi ya kuwalipa ulioitoa  mbele ya aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu.

Akitoa majibu  kwenye mkutano uliohudhuriwa na mamia ya wafanyakazi wa Tazara  mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa Trawu, Erasto Kihwele, alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omar Chambo, aliwajibu kuwa Serikali haina fedha za kuwalipa. 

Kihwele aliongeza kuwa Serikali inawasihi wafanyakazi wote wa Shirika hilo kufanyakazi kwa bidii ili mishahara yao iweze  kupatikana.


SOURCE: NIPASHE
0 Comments | Be the first to comment