|
Nani kaokota vyeti kwenye daladala?
2006-10-06 16:38:40
Na Mwandishi Wetu, Mikocheni
Wema Wilson, binti aliyehitimu masomo ya Chuo Kikuu mwaka huu, amesahau vyeti vyake halisi kwenye daladala na anaomba aliyeviokota kumrejeshea.
Akiongea kwenye ofisi za gazeti hili, Wema amesema vyeti hivyo ni vya kuhitimu kidato cha nne, cha sita katika Shule ya wasichana ya Weruweru pamoja na cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Amesema alisahau mfuko uliokuwa na vyeti hivyo kwenye daladala ya Posta-Mwenge au Mwenge-Tegeta juzi jioni.
Taarifa juu ya upotevu huo zimeripotiwa katika vituo mbalimbali vya polisi.
Ameomba yeyote aliyeona vyeti hivyo kuwasiliana na Mhariri wa gazeti hili na zawadi nono itatolewa.
|