|
Mwanamume akutwa amekufa chumbani kwake
2006-10-17 14:56:39
Na Magret Simba, Temeke
Mtu mmoja amekutwa amekufa na mwili wake ukiwa umeharibika vibaya chumbani kwake maeneo ya Kigamboni Tungi Maji, wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke Emmanuel Kandihabi amemtaja mtu huyo kuwa ni Shafii Athumani, 50.
Kamanda Kandihabi amesema mtu huyo kabla ya kufa alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya Kifua Kikuu,TB.
Amesema Kamanda Kandihabi kuwa baada ya mwili wa marehemu kufanyiwa uchunguzi na daktari wa Kituo cha Afya Kigamboni, umezikwa na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.
|