21 Oct 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Nyumba hii balaa!
 
2006-10-21 14:23:08
Na Moshi Lusonzo, Muhimbili

Ama kweli ukistaajabia ya Musa utaona ya filauni kama haya yaliyomkuta mpangaji wa nyumba moja hapa Jijini ambaye sasa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Nyumba hiyo iliyopo katika maeneo ya Jangwani Jijini Dar es Salaam masharti yake huwafanya wapangaji wajikute wakiwa kwenye wakati mgumu pale wanapokwenda kinyume na maelekezo ya baba mwenye nyumba wao.

Kijana Ahmed Maftah, 20, ni shahidi wa kile ambacho huweza kumtokea mpangaji anayeasi masharti ya kuishi katika nyumba hiyo.

Maftah amevunja kanuni mojawapo ya kumtaka mpangaji asiingize mwanamke ndani.

Baada ya kuasi masharti hayo na kuingiza demu ndani, amejikuta akiambulia kipigo kisicho cha kawaida kilichomfanya alazwe kama anavyoonekana pichani mbele.

Huku akiwa wodini na akiongea kwa shida, Maftah anasimulia sakata zima kama hivi: Siku ya tukio, kama walivyo vijana wengine wa hirimu yangu, alinitokea msichana wa wenyewe na baada ya kumsomesha vya kutosha, binti akanikubalia.

Baadaye, Maftah aliyekosa senti za kumpeleka mahala pazuri pa kujivinjari na mpenzi wake huyo, akaamua kwenda naye chumbani kwake.

”Nikamuingiza chumbani kwa kuvizia. Baadaye tukaendelea na mambo yetu. Kumbe baba mwenye nyumba aliniona wakati nikiingia na mpenzi wangu huyo.

Ndipo bila kutarajia, akanivamia ghafla chumbani na kuanza kunipiga mfululizo kama mwizi.”
Halafu ikawaje?

”Yule mpenzi wangu hakuguswa, hivyo alipata mwanya akakimbia. Mie nilipigwa sana na damu zikaanza kunivuja.

Kwa bahati, nikachoropoka na kukimbilia Kituo cha Polisi Jangwani, kisha nikaletwa hospitali na hadi sasa hali yangu nd’o kama unavyoiona,” akasema kijana huyo aliyelazwa katika wodi namba 17, Jengo la Sewahaji pale Muhimbili.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.