26 Oct 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Mtemvu ataka matumizi bora ya kisima alichozindua Tandika
 
2006-10-26 15:19:16
Na Haji Mbaruku, Jijini

Mbunge wa jimbo la Temeke, Bw.Abbas Mtemvu amezindua kisima cha maji kinachotarajiwa kupunguza tatizo la uhaba wa maji kwa wananchi wa Kata ya Azimio kule Tandika na maeneo ya jirani na eneo hilo Jijini Dar.

Wakazi wa kata hiyo waliwahi kumlalamikia mbunge huyo kuwa maji ni tatizo kubwa katika kata yao.

Bw.Mtemvu hata hivyo aliwaambia wakazi hao kuwa wawe walinzi wazuri wa kisima hicho ili kisije kikaharibika kwa muda mfupi.

”Nitashangaa sana kuona watu wameng’oa mabati na kuharibu kisima hiki,” amesema mbunge huyo ambaye pia aliwahi kuwa mkuu wa wilaya ya Nzega mkoani Tabora.

Kisima hiki ni mali yenu, mlikuwa mnasumbuka na sasa nawaombeni mkitumie vizuri ili kiweze kudumu,” amesema mbunge huyo kuwaambia wakazi wa eneo hilo wakati wa sherehe za uzinduzi.

Katika sherehe hiyo, pia Bw.Mtemvu aliwaonya baadhi ya watu wenye tabia ya kuchafua vyanzo vya maji na kusema kuwa wanastahili kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.