|
Shirikisho, Kaole kukutana Kinesi kesho
2006-12-23 13:48:24
By Mwandishi Wetu, Jijini
Timu mbili za soka za wasanii wa maigizo nchini, Shirikisho FC na Kaole SC, zinatarajiwa kukutana tena Jumapili ijayo katika mechi ya marudio ya kombe maalum la Kinesi kwenye uwanja wa Kinesi Bulls uliopo Urafiki, Jijini.
Awali timu hizo zilipokutana katika mechi ya kwanza katika uwanja huo, zilitoka sare ya bao 1-1.
Mratibu wa michuano hiyo, Joseph Itangare, amesema mshindi wa mechi hiyo atakuwa amevuka kikwazo cha kuingia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo itakayoshirikisha timu nane.
Naye mchezaji wa Shirikisho, Samson Mandieta, amesema ana uhakika timu yake itasonga mbele iwapo waamuzi watachezesha kwa haki mchezo huo.
Timu yetu ni nzuri isiyo na mamluki, hivyo tutacheza kitimu na kuweza kusonga mbele, amesema Mandieta.
|