|
Miss Utalii kusaka vipaji Krismas
2006-12-23 13:48:54
By Mwandishi Wetu, Ubungo Plaza
Jumla ya warembo 34 kutoka mikoa mbalimbali nchini, ambao watashiriki fainali ya Taifa ya Miss Utalii 2006, wataanza kinyanganyiro cha kusaka vipaji keshokutwa katika ukumbi wa Ubungo Plaza, Jijini.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Rais wa Kamati ya Miss Utalii nchini, Gideon Chipungahelo, amesema katika shindano hilo, warembo wataonyesha nyimbo mbalimbali za kiasili kwa kucheza pamoja na na kuimba.
Warembo pia watatangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika mbuga zetu mbalimbali zikiwemo Mikumi, Ngorongoro, Serengeti na Manyara, amesema Chips.
Aidha, amesema warembo hao pia watashindana Desemba 30 kuwania taji la Miss Utali Taifa, mchuano utakaofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Amesema washindi watano watakaopatikana watawakilisha nchi katika shindano la Miss Utalii Dunia huku wa kwanza akiwakilisha Miss Utalii, wapili Miss Intenati, miss milionea wa tatu, miss Bikini na miss Model.
|