28 Dec 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Risasi zarindima
 
2006-12-28 16:23:14
Na Waandishi Wetu

Kama ungetembelea kijiji cha Uyovu, kilichoko Wilaya ya Bukombe mkoani Shinyanga majuzi, ungedhani umefika eneo la mapambano kutokana na risasi zilizokuwa zikirindima.

Imeelezwa kuwa katika tukio hilo watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi walitolewa roho papo hapo.

Marehemu hao inadaiwa walizidiwa akili na wenzao wakati wakiwa kwenye mgao wa mali ya ’machumo\’ yaani mapesa waliyokomba.

Habari zaidi zinasema wahusika katika tukio hilo baadhi ni raia wa nchi jirani ya Burundi ambao ndio inasemekana walihusika na mauaji hayo.

Hata hivyo taarifa za kipolisi zinasema tayari watuhumiwa hao wametiwa mbaroni.

Imeelezwa kuwa walikutwa wakiwa na bunduki hatari aina ya FN.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyanga, Sirro Nyankoro amethibitisha tukio hilo.

Amewataja majambazi waliokamatwa kuwa ni Petro Edward, 29, George Seleman, 31, wakazi wa kijiji cha Uyovu, Gerald Mbiho,34 na Lonjino Bernado,33, wote raia wa Burundi, wanaoishi katika kijiji cha Uyovu wilayani humo.

Aidha, Kamanda Nyankoro aliwataja majambazi yaliyouawa na wenzao kuwa ni Boniface Shitta, 23 na Majaliwa Balagoma, 27 ambao nao ni wakazi wa kijiji cha Uyovu.

Amesema watu hao wamedhulumiana kiasi cha Shilingi milioni 1.5, walizokuwa wamepora hivi karibuni katika shughuli yao ya ujambazi.

Na huko Zanzibar, majambazi yenye silaha, yamepora zaidi ya Sh milioni 9.5 katika kituo cha afya.

Imeritiwa kuwa majambazi hayo yalimevamia Hospitali ya Kituo cha Afya cha kutibu ugonjwa wa kichocho kilichopo eneo la Lumumba, Zanzibar na kupora Sh. milioni 9.5.

Mkurugenzi wa Afya Jamii Zanzibar, Bw Juma Rajab, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Bw. Juma amesema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia juzi, ambapo majambazi hayo yaliezua sehemu ya paa la jengo hilo na kujitoma ndani kabla ya kupora fedha hizo.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.