24 Apr 2007 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Maendeleo ya Sada
 
2007-04-24 17:34:49
Na Mwandishi Wetu

Bi. Mwanaidi Mwesi, 17, ambaye aliomba msaada wa pesa kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake, Sada anatarajia kupokea pesa zilizochangwa hadi sasa leo katika ofisi za gazeti hili zilizoko Mikocheni, Jijini.

Mama huyo alitua Jijini jana jioni akitokea Moshi baada ya kupewa taarifa kwamba wasamaria wema wamemchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya mwanae.

Mtoto Sada anasumbuliwa na matatizo ya kupumua baada ya kuzaliwa bila kuwa na pua, hali hiyo imemfanya aishi kwa shida kubwa huku mama yake akiwa hana msaada wowote.

Baba yake Sada alitimka baada ya mkewe kujifungua mtoto mwenye matatizo ya kiafya.

  • SOURCE: Alasiri
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.