|
Wakulima kuanzisha benki
2008-02-26 15:40:36
Na Azizi Issa
Mtandao wa wakulima wa Dunduliza, unatarajia kauanzisha benki ya mazao kwa lengo la kuwasaidia wakulima kupata mikopo ya fedha na pembejeo.
Mshauri wa Kilimo wa mtandao huo, Bw. Rodgers Masha amesema jambo hilo litawasaidia kunufaika na fedha na pembejeo, jambo ambalo linamekuwa likizishinda taasisi za kifedha kwa sababu ya hofu ya kuogopa kutorejeshewa fedha zao.
Akasema kuanzishwa kwa benki hiyo kutawanufaisha wakulima wengi na kuwaondolea tatizo la ukosefu wa soko kwa mazao na pembejeo.
Pia akasema kuanzishwa kwa benki hiyo kutawawezesha wakulima kupata mafunzo mbalimbali yanayohusika na kilimo.
Akasema tafiti mbalimbali zilizowahi kufanyika wilayani Mbarali mkoani Mbeya zimeonyesha wakulima hawazalishi kwa tija, jambo ambalo linawafanya kushindwa kufikia malengo waliyoyapanga.
|