|
Mwanaume Dar ajiua kwa kitanzi
2008-03-17 19:05:47
Na Usu-Emma Sindila, Jijini
Mtu mmoja amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali alioanza kwa kuutundika mtini kabla ya kujining\'iniza hadi kufa.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Jamal Rwambow ameiambia Alasiri leo asubuhi kwa njia ya simu kuwa, mtu huyo ametambulika kwa jina la Said Kambawene, 30, fundi maarufu wa baiskeli.
Kamanda Rwambow amesema tukio hilo limetokea jana mishale ya saa 12:00 jioni katika eneo la Makongo Juu.
Amesema marahemu hakuacha ujumbe wowote lakini siku tatu zilizopita, alimsafirisha mkewe kwenda kijijini kwao Mwalusembe katika wilaya ya Mkuranga.
Kamanda Rwambow amesema polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo na mwili wa marehemu umehhifadhiwa katika hopsitali ya Mwananyamala.
|