14 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Sportsnews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Yanga fc nao wachokozana
 
2008-05-14 15:21:16
By Onesmo Kapinga, Jijini

Wanachama wa klabu ya soka ya Yanga wamemwashia `moto` Katibu Mipango ya Klabu hiyo, Patrick Fata na kumtaka ajiuzulu wadhifa wake.

Wanachama hao wanataka kiongozi huyo ajiuzulu kwa vile ameshindwa kutimiza majukumu yake kama kiongozi.
Akiongea kwa niaba ya wanachama wenzake wanaotaka mabadiliko hayo, Haruna Athuman (0176) , alimtuhumu kiongozi huyo kushindwa kuleta maendeleo klabuni hapo.

``Hakuna mipango ya maendeleo klabuni, anafanya nini sas? kwanini asijiuzulu?`` alihoji mwanachama huyo.

Athuman alisema kuwa wanachama wanashangaa kuona Fata anafanya kazi za uhazini wakati ni kinyume na utaratibu.

  • SOURCE: Alasiri
TODAY
-----------------------------------------------
Editorial
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.