|
Wakulima Rukwa wanolewa
2008-05-14 15:58:55
Na Azizi Issa
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa imeanza mpango kabambe wa kutoa mafunzo kwa wakulima ili kuwaondoa katika kilimo kisicholeta tija.
Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa halamashauri hiyo, Bw. Antony Mwambene mafunzo hayo ni sehemu ya mkakati wa kuendesha mafunzo ya shamba darasa katika vijiji vyote 169.
Akasema wilaya hiyo ina mabwana shamba wapatao 45 jambo ambalo halitoshelezi mahitaji ya wakulima wanaohitaji huduma yao ili kuondokana na kilimo duni.
Akasema halmashauri hiyo ina jumla ya vijiji 169 na kwamba mafunzo hayo yanaendeshwa kwa sasa katika vijiji 10 kwa kuwashirikisha baadhi ya wananchi.
Akasema mafunzo hayo yanayoanzia na kuandaa shamba hadi uvunaji wa zao husika, yanalenga katika kuwafanya wawe wataalamu wa kilimo waliobobea.
|