|
Wakulima kuneemeka
2008-05-17 15:13:39
Na Azizi Issa
Huenda wakulima wakaanza kuneemeka mara baada ya Serikali, kukamilisha ufumbuzi wa tatizo la masoko ya mazao yao.
Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Bi. Celina Kombani serikali imeanza mchakato wa kutafuta masoko ya mazao yao.
Akasema hatua hiyo inalenga katika kupunguza na kama si kumaliza kabisa tatizo la masoko kwa mazao yao ya kilimo.
Akasema ugumu ambao wamekuwa wakiupata wakulima umekuwa ukiwakwaza katika shughuli za uzalishaji.
Aidha, akizungumzia kuhusiana na kukosekana kwa mbolea za ruzuku katika mkoa wa Tabora, Waziri huyo akasema serekali inakusudia kurejesha utaratibu wa kutoa mbolea ya ruzuku kwa wakulima.
|