|
Madonna amekanusha taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari
2006-10-06 15:58:21
Na EAR Habari
Mwanamuziki maarufu wa muziki wa pop wa Marekani, Madonna, amekanusha taarifa zilizotolewa na vymbo vya habari, kwamba na mpango wa kutaka kuchukua Mtoto wa kiume kwa nia ya kumlea, nchini Malawi.
Akiongea na shirika la Habari la AP, msemaji wa mwanamuziki huyo Liz Rosenberg, amesema kwamba mwanamuziki huyo hajachukua mtoto wa kiume, kama taarifa za hapo awali zilivyodai, ambapo amedai kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote.
Rosenberg amesema kwamba Mwanamuziki huyo yuko nchini Malawi kwa ziara binafsi, ambapo anashiriki katika ujenzi wa kituo cha kulelea watoto yatima, pamoja na mipango mingine ya kusaidia watoto, waliopoteza wazazi wao kutokana na ugonjwa wa ukimwi.
Hivi karibuni Maafisa wa serikali ya Malawi, walidai kwamba Madona yuko katika harakati za kutuma maombi, ya kuchukua mtoto wa kiume nchini humo.
|