31 Dec 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Kipindupindu chauwa wafungwa wanne Uganda
 
2006-12-31 15:44:40
Na EAR Habari

Wafungwa wanne katika gereza la Kabasanda wilayani Mpigi nchini Uganda wamekufa, kutokana na ugonjwa wa kipindupindu uliolikumba gereza hilo.

Kwa mujibu wa mkuu wa gereza hilo, Bw. Lawrence Buserezi mmoja wa wafungwa hao amekufa akiwa njiani kuelekea nyumbani baada ya kumaliza kifungo chake.

Hata hivyo vyanzo vya habari nchini Uganda vimedai kwamba chanzo cha mlipuko wa ugonjwa huo katika gereza hilo ni msongamano uliopo gerezani hapo, pamoja na hali ya uchafu iliyokithiri.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.