29 Apr 2007 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Mahabusu wapatao 10,040 wanashikiliwa Uganda bila kesi zao kutajwa
 
2007-04-29 15:05:07
Na EAR Habari

Habari kutoka Uganda, zinasema kuwa mahabusu wapatao 10,040, wanashikiliwa magerezani, kwa muda mrefu, bila ya kesi zao kutajwa mahakamani.

Taarifa zaidi zimesema, mamia ya mahabusu nchini humo, wapo kizuizini kwa zaidi ya kipindi cha mwaka mmoja hadi mitano, bila ya kesi zao kufikishwa mahakamani.

Miongoni mwa mahabusu hao, ni wanaokabiliwa na kesi za mauaji, kesi za wizi, kesi za ulawiti, ubakaji, uhalifu mdogo mdogo, pamoja na kesi za mauaji yasiyo kusudiwa.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.