23 Mar 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Jeshi la Sudan limeikosoa ripoti ya Umoja wa Mataifa
 
2008-03-23 15:12:57
Na EAR Habari

Jeshi la Sudan limeikosoa ripoti ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa, iliyolishutumu jeshi hilo kuhusuka na vitendo vya kubaka wanawake na wasichana, na kuvamia na kupora katika miji wakati wa mashambulizi huko magharibi katika jimbo la Darfur.

Msemaji wa jeshi la Sudan pia amekanusha ripoti za Umoja wa Mataifa, kuwa uvamizi uliofanya kwa njia ya anga na majeshi ya ardhini katika miji mitatu mnamo mwezi februari, ulisababisha vifo vya watu 115.

Brigedia Jenerali Osman Mohamed al-Aghbash, amesema jeshi linatekeleza wajibu wake wa kuwalinda raia kwa kuwafukuza waasi.

Aidha amewalaumu waasi wa huko Darfur kwa kuwashambuliwa raia, na kupora mali zao.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.