|
Wazazi Kenya wataka kuanzishwa kwa bodi ya mitihani
2008-03-23 15:15:35
Na EAR Habari
Chama cha Taifa cha Wazazi nchini Kenya kimeliomba Baraza la Taifa la Mitihani nchini humo, kuanzisha bodi ya mitihani.
Chama hicho cha Wazazi kimesema utendaji wa baraza hilo umeingia dosari, kutokana na namna baraza hilo lilivyosimamia mitihani ya kumaliza elimu ya sekondari
Nchini humo mwaka jana.
Wito huo wa chama cha wazazi umetolewa kufuatia kutakiwa kutolewa upya kwa matokeo ya mitihani ya zaidi ya wanafunzi elfu 4, kwa kile baraza la taifa la mitihani lilichokiita kukosewa kwa gredi zilizotolewa.
|