24 Mar 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Shule ya biashara Makerere yalumbana na wizara yab elimu
 
2008-03-24 16:52:57
Na EAR Habari

Shule ya Biashara katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, imeingia katika malumbano na wizara ya elimu kuhusiana na utaratibu wa uteuzi wa wafanyakazi wake.

Shule hiyo inaishutumu wizara kupitia tume ya watumishi wa elimu, kwa kutangaza nafasi ya naibu makamu wa chuo bila ya kuhusishwa.

Baraza la shule hiyo limepinga tangazo la ajira lililotolewa na wizara, kwa madai kuwa jukumu hilo ni lao, kwani makamu huyo wa shule ya biashara atakuwa muajiriwa wao.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.