24 Mar 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Marekani yalegeza tahadhari ya raia wake kutosafiri Kenya
 
2008-03-24 16:54:42
Na EAR Habari

Marekani imetoa taarifa ya kulegeza tahadhari ya kuto safiri nchini Kenya, ambayo imeeleza kuwa ghasia zimepungua mno nchini humo, baada ya kufikiwa makubaliano ya kugawana madaraka.

Taarifa hiyo imepokelewa vyema na sekta ya utalii ya Kenya, ambayo imeanza kuzaa matumaini ya kupata watalii zaidi kutoka Marekani.

Hata hivyo taarifa ya tahadhari ya usafiri, imewaonya raia wa Marekani watakaotembelea Kenya kuwa waangalifu, ili kuepuka uwezekano wa kukabiliwa na vitendo vya uhalifu.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.