|
Jitihada zinaendelea kuwafutia kesi wanafunzi wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam
2008-05-08 14:29:13
Na EAR Habari
Wakati uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nchini Tanzania, ukiwa katika jitihada za kufuta kesi inayowakabili wanafunzi wake waliosimamishwa masomo kwa kutuhumiwa kufanya vurugu mwezi uliopita, imeelezwa kuwa sheria hairuhusu kufanya hivyo.
Vyombo mbalimbali vya habari vimemkariri Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Yunus Mgaya, akiwataka wanafunzi hao kurejea chuoni kwa maandalizi ya kufanya mitihani inayotarajiwa kuanza Mei 19 mwaka huu.
Lakini mwanasheria katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu amesema kwamba, mamlaka yenye uwezo wa kufuta kesi ya jinai ni Jamhuri ya Muungano.
|