08 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Watimishi wa serikali nchini Kenya kupewa nyongeza ya mishahara
 
2008-05-08 14:30:54
Na EAR Habari

Waziri wa utumishi nchini Kenya Mh. Dalmas Otieno, amesema kwamba serikali itatoa shillingi billioni 3.5 ikiwa ni nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa serikali, kuanzia mwezi julai ili kuwa na uwiano.

Fedha hizo zitatumika kwa kuandaa utaratibu mpya uliobuniwa na bodi ya utumishi wa umma ya mishahara, ili kuhakikisha kuwa kuna uwiano sawa wa mishahara kwa watumishi wa serikali.

Habari zinasema ingawa waziri hakutangaza asilimia atakayopata mfanyakazi wa kima cha chini, lakini kutolewa kwa fedha hizo kunamaanisha kuongezeka kwa mishahara kwa watunmishi wa kiwango cha A mpaka M.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.