09 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Ashikiliwa na polisi Tanzania kwa kusafirisha Wasomali wasio na vibali
 
2008-05-09 16:37:04
Na EAR Habari

Jeshi la Polisi nchini Tanzania linamshikilia mkazi wa Himo Moshi, Mkoani Kilimanjaro, William Makina baada ya kukutwa akisafirisha raia 34 wa Somalia ambao hawakuwa na vibali vya kuingia wala kuishi nchini.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, nchini Tanzania Thobias Andengenye, zilisema Makina, alikamatwa jana, majira ya jioni na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani katika eneo la Dumila wilayani Kilosa, katika barabara kuu ya Morogoro-Dodoma.

Alisema mtuhumiwa huyo alikuwa akiendesha lori aina ya Fuso namba T 315 ADM lililokuwa likitokea Kiteto mkoani Manyara kuelekea jijini Dar es Salaam na kwamba dereva huyo na raia hao wa Kisomali watafikishwa mahakamani baada ya taratibu za upelelezi kukamilika.

  • SOURCE: EAR
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.