|
Waziri wa jinsia na watoto Kenya ataka kuanzishwa sheria mpya ya watoto
2008-05-09 16:37:56
Na EAR Habari
Waziri wa jinsia na watoto nchini Kenya Esther Murugi, ametaka kuanzishwa kwa sheria mpya ya watoto wenye uhitaji nchini Kenya na akasema kwamba kwa sasa serikali inandaa sera itakayo ainisha hatima ya watoto yatima.
Amesema kwamba sheria zilizopo zinazohusiana na yatima na watoto hazitoshelezi na zimekuwa zikiwabagua,kuwapuuza ikiwa ni pamoja na kuwanyanyapaa.
Waziri Murugi amesema watoto yatima wanakabiliwa na matatizo ya kukosa chakula,nyumba bora,fedha za kuendeshea maisha yao ikiwa ni pamoja na elimu na huduma za afya.
|