|
Vikosi vya askari wa Ethiopia vyasambaza chakula walichonunua wenyewe
2008-05-15 17:17:57
Na EAR Habari
Vikosi vya askari wa Ethiopia walioko katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu, wamesambaza msaada wa chakula walichonunua wenyewe kwa mishahara yao.
Karibia magunia mia 4 ya mtama yamekabidhiwa kwa watu wasiopungua mia 5 katika wilaya ya kusini ya Baynile.
Umoja wa Matifa umesema zaidi ya theluthi ya raia wa Somalia wanategemea msaada kutoka nje, na kuwa wale masikini waliopo mijini wanapata shida kupata chakula.
|