|
Sheria mpya za kazi zaleta tija nchini Tanzania
2008-05-15 17:18:23
Na EAR Habari
Utekelezaji wa sheria mpya za kazi nchini Tanzania, umepunguza muda uliokuwa unatumika kushughulikia migogoro inayojitokeza sehemu za kazi, na hivyo kuongeza tija makazini.
Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Bibi Edin Mangesho, amesema sheria hizo zinatoa siku 30 kwa wasuluhishi kutoa ufumbuzi wa haraka wa migogoro inayojitokeza sehemu za kazi.
Amesema migogoro sehemu za kazi imepungua, tangu utekelezaji wa sheria hizo ulipoanza takriban miaka miwili na nusu iliyopita.
|