|
Watumishi wa umma Kenya wapokea barua za kuchangia watu waliotawanyika
2008-05-15 17:18:48
Na EAR Habari
Watumishi wa umma nchini Kenya wamepokea barua zinazowataka kuchangia mfuko uliozinduliwa hivi karibuni, wa kuwasaidia kurejea kwenye makazi yao watu waliotawanyika.
Mkuu wa Huduma za Jamii Francis Muthaura, amewaandikia makatibu wakuu wote akiwataka waombe michango kutoka kwa wafanyakazi wao, kwa ajili ya mfuko huo unaolenga kukusanya bilioni 30, za kuwasaidia wahanga wa vurugu zilizozuka nchini humo mara baada ya uchaguzi.
Baadhia ya barua hizo zimeainisha kabisa kiwango cha chini mtu anachotakiwa kuchangia, kutokana na kazi yake na cheo alicho nacho.
|