|
Shea ya chakula kwa wanafunzi wa chuo cha Makerere yapunguzwa
2008-05-15 17:19:13
Na EAR Habari
Ongezeko la bei ya chakula limevuruga bajeti ya Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, na kusababisha utawala wa chuo hicho kupunguza shea ya chakula kwa wanafunzi.
Pamoja na kupunguza kiwango cha mlo unaotolewa, chuo hicho pia kimebadili aina ya chakula kinachotolewa.
Mkuu wa Wanafunzi John Ekudu, amefafanua kuwa chuo hicho kinafanya kila jitihada kumaliza tatizo hilo, na kuhakikisha wanafunzi hawali chakula cha aina moja kwa muda mrefu.
Hivi sasa wanafunzi hao wanapatiwa ugali na maharagwe tu badala ya vyakula mchanganyiko.
|