10 Jul 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Sportsnews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Mashindano ya mpira wa kikapu kwa vijana chini ya umri wa miaka 14 na 18 yamemalizikia
 
2006-07-10 11:49:53
By ITV Habari

Mashindano ya mpira wa kikapu kwa vijana chini ya umri wa miaka 14 na 18 yamemalizikia jana jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wa wasichana chini ya umri wa miaka 14, ubingwa umechukuliwa na timu ya Ali Hassan Mwinyi baada ya kuifunga timu ya Don Bosco vikapu 10-3.

Kwa upande wa wavulana chini ya umri wa miaka 14 ubingwa umechukuliwa na Don Bosco baada ya kuifunga JKT vikapu 24-14 na kwa upande wa wavulana chini ya umri wa miaka 18 ubingwa umechukuliwa na TM Rocekts baada ya kuifunga Don Bosco vikapu 45-26.

Mashindano hayo yameandaliwa na chama cha mpira wa kikapu mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na shirika la michezo kwa vijana- Emima yalishirikisha jumla ya timu 18 za shule za msingi pamoja na vilabu.

  • SOURCE: ITV
TODAY
-----------------------------------------------
Editorial
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.