26 Mar 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Sportsnews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Zanzibar yashinda mashindano ya NSSF Pasaka
 
2008-03-26 15:32:42
By ITV Habari

Timu za mpira wa pete na soka za shirika la hifadhi ya jamii la Zanzibar- ZSSF- zimeibuka washindi wa michuano ya bonanza la pasaka baada ya kuzilaza timu za shirika la hifadhi ya jamii la taifa Tanzania bara- NSSF, katika michuano iliyochezwa mjini arusha.

Katika michuano hiyo timu ya soka ya ZSSF imeibuka mshindi kwa njia ya penati baada ya kuifunga timu ya NSSF kwa mabao 7 - 2 baada ya dakika 90 kuma kwa sale ya mabao 2- 2 ambapo kwa upande wa mpira wa pete timu hiyo ya zssf imefanikiwa kuilaza timu ya nssf kwa mabao 27 - 14.

Akikabidhi zawadi ya vikombe kwa washindi mgeni rasmi katika Bonanza hilo chiku matessa amesema michezo hiyo ambayo imekuwa ikifanyika kila mwaka imekuwa ikijenga undugu baina ya mashirika hayo na kutoa wito kwa mashirika mengine kuiga mfano huo.

  • SOURCE: ITV
TODAY
-----------------------------------------------
Editorial
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.