|
Nchi za Afrika zitaathirika zaidi kutokana na mabadiliko ya tabia nchi
2008-05-15 11:09:01
Na ITV Habari
Nchi za Afrika zitaathirika zaidi kutokana na mabadiliko ya tabia nchi licha ya kuchangia kidogo sana katika tatizo hilo ambalo athari zake ni pamoja na ukame, mafuriko na vimbunga.
Mkurugenzi wa mazingira katika ofisi ya makamu wa rais Bw. Erick Mugurusi amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia maadhimisho ya siku ya mazingira yanayofanyika Juni 5 kila mwaka ambapo amesema kazi iliyopo ni kwa nchi za afrika kushiriki katika kuzishinikiza nchi zilizoendelea kupunguza uzalishaji wa gesi ili kuepusha athari zake.
Kauli mbiu ya mwaka huu kidunia ni badili mazoea , jenga uchumi endelevu kwa kudhibiti uzalishaji gesi joto- huku kauli mbiu ya kitaifa ni hifadhi mazingira , dhibiti uchomaji moto, panda miti.
|