15 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Leo ni siku ya wanafamilia
 
2008-05-15 11:10:14
Na ITV Habari

Leo ni siku ya wanafamilia ambapo watanzania wameshauriwa kuwa na mshikamano miongoni mwa familia zao ili waweze kukabiliana na hali ngumu zinazozikabili familia katika jamii.

Ushauri huo umetolewa na waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia na watoto Mh. Magreth Sitta ambaye amesema serikali katika kujali suala la wanafamilia imechukua hatua za kuzisaidia familia nchini kwa kutunga sera ya kukabiliana na matatizo ya kijamii hasa la kupiga vita mila desturi na tamaduni zilizopitwa na wakati.

Sherehe ya wanafamilia inaadhimishwa katika ngazi ya mkoa ikiwa na kauli mbiu inayosema kina baba na familia majukumu na changamoto.

  • SOURCE: ITV
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.