|
Wafanyabiashara 60 wa Tanzania kufanya ziara A. Mashariki
2008-05-16 14:25:02
Na ITV Habari
Ujumbe wa wafanyabiashara 60 kutoka Tanzania unatarajia kufanya ziara za kibiashara katika nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka huu kwa ajili ya kujifunza.
Waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Diodorus Kamala amesema ziara hiyo itasaidia wafanyabiashara hao kutambua soko la Afrika Mashariki kupanua biashara ya Tanzania pamoja na kufahamu njia zinazotumiwa na watanzania wenzao kuvutia uwekezaji na kuwataka wafanya biashara wa tanzania kuchangamkia fursa hiyo na kuwa tayari kuthubutu katika biashara.
|