|
Hospitali ya misheni Iambi inakabiliwa na upungufu wa watumishi
2008-05-16 14:28:49
Na ITV Habari
Hopitali ya misheni Iambi iliyopo kata ya Nkungi wilayani Iramba inakabiliwa na upungufu wa watumishi arobaini wa kada ya uuguzi hali inayochangia baadhi ya huduma katika hospitali hiyo kutotekelezwa kwa ukamilifu.
Wauguzi wa hospitali hiyo inayomilikiwa na kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania -KKKT Dayosisi ya kati wamemwambia askofu wa dayosisi hiyo kuwa kwa sasa ina idadi ndogo ya watumishi ikilinganishwa na mahitaji ya huduma ambayo ni mara mbili ya wauguzi arobaini waliopo hivi sasa.
Kwa upande wake askofu wa dayosisi hiyo askofu Eliuphoo Sima amewataka watumishi kutoa huduma kwa kuzingatia upendo, huruma na kuacha tabia ya kubagua watumishi kwa makabila huku akitaka wenye viwango vya chini vya elimu wajiendeleze wakiwa kazini kuboresha taaluma zao.
|