|
SUMATRA wapiga marufuku daladala kupandisha nauli Dar
2008-05-16 14:34:50
Na ITV Habari
Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu - SUMATRA imepiga marufuku upandaji holela wa nauli za mabasi ya abiria jijini maarufu kama daladala zinazofanya safari zake katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
Marufuku hiyo imetolewa na afisa mfawidhi wa SUMATRA kanda ya mashariki Bw. Walakani Luhamba kufatia msako wa kushtukiza uliofanywa na mamlaka hiyo na kukamata daladala korofi zinazotoza nauli kinyume na utaratibu.
Baadhi ya wakazi wa jiji wamekiri kuwepo kwa ongezeko holela la nauli huku baadhi ya makondakta wakidai tatizo hilo linachangiwa kwa kiasi kikubwa na msongamano barabarani.
|