28 Oct 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Basi lateketea
 
2006-10-28 08:13:28
Na Nashon Kennedy, Mwanza

Basi la Kampuni ya Mohamed Trans, limeteketea kwa moto katika eneo la Buhongwa, wakati likiwa njiani kutoka Mwanza kuelekea Kahama, mkoani Shinyanga. Lilikuwa na abiria 60.

Mwandishi wa habari hizi aliyekuwa kwenye msafara wa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, alishuhudia wananchi pamoja na wajumbe wa kamati hiyo, wakijaribu kuzima moto huo bila mafanikio.

Moto huo ulianza saa 7:00 mchana na kudumu kwa dakika 15, ambapo askari wa kikosi cha zimamoto kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, walifika katika eneo la tukio kusaidia kuuzima moto huo.
Hata hivyo, jitihada hizo hazikufanikiwa na basi hilo likateketea.

Dereva na kondakta, ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja, walitoweka.

Hata hivyo, abiria wote 60 walinusurika na chanzo cha moto huo, hakikuweza kujulikana.

  • SOURCE: Nipashe
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.