24 Oct 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Wakulima wa zao la pamba msipokee madawa yaliyochelewa
 
2006-10-24 14:09:29
Na Radio One Habari

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Brigedia Jenerali mstaafu Yohana Balele amewataka wakulima wa zao la pamba wasipokee madawa yaliyochelewa kutolewa na bodi ya pamba ili kuepuka hasara na usalama wa maisha yao.

Kauli yake inafuatia malalamiko ya wakulima wa zao hilo wilayani Maswa juu ya tabia ya bodi hiyo kuwapelekea madawa katika kipindi cha Aprili, Mei na Juni majira ambayo vitumba vya pamba huwa vimekomaa tayari kwa mavuno ya pamba na dawa kutotumika katika kipindi hicho.

Amesema ni hasara kwa mkulima kupokea madawa hayo katika kipindi ambacho hayatatumika na kwamba ni hatari kwa maisha na familia yake kukaa nayo ndani ya nyumba kwa vile madawa hayo ni sumu na yanahitaji utunzaji wa kifamasia.

Mkuu huyo wa mkoa wa Shinyanga alikuwa akizungumza kwa nyakati tofauti na wakulima wa vijiji vya tarafa za Nhungu, Sengerema na Mwanga wilayani Maswa.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.