25 Oct 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Waislamu wametakiwa kudumisha mshikamano
 
2006-10-25 14:55:06
Na Radio One Habari

Waislamu nchini wameshauriwa kuendeleza mshikamano na uadilifu kama walivyofanya wakati wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Sheikh wa Msikiti wa Wilaya ya Songea Mjini, Ustaadh Shaibu Mohamed ametoa changamoto hiyo katika salamu zake za sikukuu ya Eid-El-Fitr.

Ustaadh Mohamed amesema ni vyema waislamu wakadumisha mshikamano na umoja wa kijamii baina yao na hata waumini wa dini zingine.

Amewataka Waislamu kusherehekea Eid kwa furaha na kuwasaidia wote wenye shida na baada ya hapo waendelee kufanya kazi kwa bidii na maarifa.


  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.