22 Apr 2007 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Vijiji kupatiwa mashine za kufyatua matofali
 
2007-04-22 15:26:25
Na Radio One Habari

Baadhi ya halmashauri za mkoa wa Shinyanga zimeanza kusambaza mashine za kufyatulia matofali zenye gharama nafuu kwa lengo la kuwawezesha wananchi wa vijijini kujenga nyumba bora na kuondokana na nyumba duni.

Mashine hizo zimetengenezwa maalum kwa ajili ya kufyatua matofali ya udongo, saruji na ya kuchoma.

Wakitoa taarifa hizo kwa nyakati tofauti wakurugenzi watendaji wa halmashauri za Meatu, Bariadi na Kahama wamesema zoezi la kugawa mashine hizo limeanza katika kata za halmashauri.

Mmoja wa Wakurugenzi hao , Bw. Paul Chiwele wa halmashauri ya Meatu amesema mashine hizo tayari zimesambazwa katika kata za tarafa tatu ambako wananchi watajifunza jinsi ya kuzitumia na kufyatua matofali kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zenye gharama nafuu.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.