|
Waandishi lindeni maslahi ya taifa
2007-04-29 15:24:09
Na Radio One Habari
Waandishi wa habari wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi na maadili ya taaluma sanjari na kulinda maslahi ya taifa kwa mataifa mengine.
Wito umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Morogoro Bw, Saidi Mwambungu wakati akifungua mkutano wa siku moja wa wadau wa habari kutoka mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Lindi na Morogoro.
Amesema vyombo vya habari vina wajibu wa kuandika na kukosoa yanayostahili kukosolewa kwa maslahi ya wananachi na taifa kwa ujumla lakini viepuke habari zisizofanyiwa kazi kwa kina ambazo mara kadhaa zimekuwa zikizua migogoro ama kukidhalilisha chombo husika.
Mkutano huo uliandaliwa na Baraza la habari Tanzania -MCT- na umoja wa vyama vya waandishi wa habari vya mikoa –UTPC- kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau juu ya mapendekezo kuhusu muswada wa sheria ya uhuru na haki ya kupata habari ya mwaka 2007.
|