|
Sheria itakayoongoza mifuko ya hifadhi ya jamii kuundwa
2007-04-30 15:47:56
Na Radio One Habari
Serikali iko mbioni kuandaa rasimu ya sheria itakayoongoza utendaji wa shughuli za mifuko ya hifadhi ya jamii hapa nchini ili kuondoa kasoro za utendaji zilizopo hivi sasa.
Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo, amesema sheria hiyo itasaidia pia utekelezaji wa sera ya taifa ya hifadhi ya jamii ya mwaka 2003 inayopendekeza kuundwa kwa chombo kimoja kitakachosimamia mifuko yote.
Bwana Luhanjo alikuwa akizungumza wakati wa warsha ya makatibu wakuu wa wizara za serikali kuhusu uboreshaji wa mifuko hiyo hapa nchini.
Nao baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wamesema iwapo sheria hiyo itaundwa itasaidia kupunguza kasoro zilizopo ndani ya mifuko ya hifadhi ya jamii.
|