|
Miradi ya maji yagharimu zaidi ya shilingi milioni 32 mikoa ya Singida, Shinyanga na Tabora
2008-03-24 16:56:46
Na Radio One Habari
Zaidi ya shilingi milioni 32-na-laki-7 zimetumika kwa ajili ya miradi ya maji katika mikoa ya Singida, Shinyanga na Tabora.
Fedha hizo zimetumika kupima mabwawa manne mkoani Shinyanga na kufanya utafiti wa upatikanaji wa maji ardhini katika vijiji 31 vya mikoa ya Tabora na Singida.
Afisa wa Bonde la Kati lenye makao yake makuu mjini Singida Bwana Mtoi Kanyawanah ameyasema hayo wakati akiwasilisha taarifa yake ya utendaji kazi kwenye kikao cha bodi.
Amefafanua kuwa baada ya utafiti huo maandalizi yote yamekwisha kamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa utekelezaji wa miradi hiyo wakati wowote.
Amesema lengo ni kuhakikisha kuwa wananchi katika maeneo hayo wanapata huduma ya maji safi na salama kwa ajili ya matumizi ya majumbani na mifugo yao.
|