24 Mar 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Mpango wa kupambana na malaria wazinduliwa Ruvuma
 
2008-03-24 17:00:45
Na Radio One Habari

Wadau wa sekta ya afya Mkoani Ruvuma wametakiwa kuelekeza zaidi nguvu zao katika kupambana na ugonjwa wa malaria ambao kwa sasa unachangia vifo vingi vya watoto na wajawazito mkoani humo.

Changamoto hiyo imetolewa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bwana Claudio Bitegeko alipozindua mpango wa Milenia wa kupambano na ugonjwa wa Malaria mkoani humo unaotekelezwa na mashirika yasiyo ya kiserikali ya Ores Tanzania na COTN.

Amesema elimu zaidi inahitajika kwa wananchi ili kuweza kupambana na Malaria unasababisha vifo vingi vya watoto na wajawazito.

Akisoma risala ya mashirika hayo mawili Mratibu wa mradi huo Bwana Max Mahudi alisema shirika la ORES Tanzania mbali ya kuendesha mapambano dhidi ya Ukimwi pia limeamua kujikita katika vita dhidi ya Malaria.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.