04 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Mfuko wa Bima ya Afya kujenga hospitali kubwa Dar
 
2008-05-04 23:15:52
Na Radio One Habari

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya unakusudia kujenga hospitali kubwa jijini Dar es Salaam ili kutoa huduma za matibabu na za uchunguzi kwa wanachama wa mfuko huo na wananchi wengine.

Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo Bwana Emanuel Humba imesema hospitali hiyo itatoa matibabu ya Daraja la kwanza na itakuwa na huduma zote muhimu.

Bwana Humba amesema kwa sasa Mfuko wake unawasiliana na mamlaka mbali mbali za Serikali pamoja na wadau wengine ili kupata eneo kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo, uamuzi ambao tayari umesharidhiwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko huo.

Hivi karibuni Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulitoa Shilingi Milioni 255 kwa ajili ya kukarabati sehemu za kutolea huduma katika hospitali za Muhimbili, Mwananyamala, Amana na Temeke, ikiwa ni juhudi za Mfuko huo kuboresha huduma za matibabu Jijini Dar es Salaam.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.